November 19, 2015


Zaidi ya Ekari 20 za msitu wa Hifadhi ya jamii wa wananchi wa Kikunguni Shumba Viamboni, Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba zateketea na moto.
Moto huo umeiunguza zaidi ya miti 588 mikubwa, imeunguwa moto katika msitu huo ikiwemo Mivule, Mbamba kofi , Mikorosho, Mitondoo , Mifuu , Michocha, Mizambarau Sali, ambayo ingekatwa na kuuzwa kisheria zingepatikana zaidi ya shilingi Milioni 20.
Msitu huo wenye ekari 50 umekubwa na majanga hayo, baada ya watu wasiojulikana kupiga tanu ya mkaa na kuacha moto chini, uliosambaa katika msitu huo wa jamii.
IDARA ya Misitu na Mali zisizorejesheka Pemba, imesema imesikitishwa na kitendo kilichofanywa na watu wasio julikana, kuchoma moto msitu wa wanajamii wa Kikunguni Shumba Viamboni
Mkuu idara hiyo harif Faki Sharif, amesema athari iliyopatikana ni  kubwa  kwa kupoteza miti adimu sana, pamoja na suala la kimazingira.
 “Athari lazima zitakuwepo na wala hazikosekani, kama unavyojuwa miti ina mambo mengi muhimu, nadhani katika mvua hizi zinazoendelea kunyesha basi hali ya asili inaweza kurudi japo kuwa si kwa kasi kubwa”amesema.
Amewataka wananchi kuwapiga vita watu wanaopiga tanu za mkaa, karibu na misitu huo au karibu na majumba ili kudhibiti athari itakayoweza kujitokeza baadae.

0 comments:

Post a Comment