November 19, 2015


Waziri Mkuu mteule wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh Kassim Majaliwa amesema hakuwa na taarifa yeyote juu ya uteuzi wake uliofanywa na Rais.
Majaliwa amedai usiri uliotumika ni mkubwa ambao hata yeye atauendeleza katika kuimarisha Serikali.
“Huwezi amini mpaka asubuhi nafanya zoezi na Wabunge wenzangu sikuwa najua lolote, mimi ni kocha wa timu ya mpira ya Bunge”
"……Yani mpaka Spika ameanza na ile Ruangwa nikapigwa na butwaa, na nimelia kwa sababu sikuamini kilichotokea, ila ndo hivyo Rais ameniamini akanipa nafasi” alisema Majaliwa alipokuwa akizungumza na Azam TV.

0 comments:

Post a Comment