November 17, 2015



WANAFUNZI 151 wengi wao chini ya umri wa miaka 18 wamelazimika kukatishiwa masomo yao baada ya kufungishwa ndoa hapa Zanzibar katika kipindi cha miaka minne.
Taarifa ya Wizara ya elimu iliyotolewa na  Mrajisi wa elimu Zanzibar Siajabu Makame Pandu, zinaeleza kuwa idadi hiyo ni wale walioripotiwa, mara baada ya kuolewa kuanzia mwaka 2011 hadi mwezi septemba mwaka huu .
Kwa mujibu wa taarifa hiyo mwaka 2011 kuliripotiwa wanafunzi 53, wakati mwaka 2012 wanafunzi 50 huku mwaka 2013 walifikia watoto 29 huku mwaka 2014 wanafunzi 18 wameripotiwa kuolewa.
Wilaya ya Micheweni ilikuwa ikiongoza kuwa na idadi ya wanafunzi 62, ikifutiwa wilaya za Wete Pemba na Kati kwa unguja wanafunzi 19, chini ya wilaya Magharibi iliokuwa na watoto 17, huku wilaya za Chake chake na Mkoani zikiwa na wanafunzi 14 kila wilaya.
Mrajisi wa elimu Zanzibar Siajabu Makame Pandu, amesema ndoa za utotoni zimekuwa zikiathiri sana maendeleo ya watoto wa kike kielimu, jambo linalowavunjia mipango na mikakati yao ya baadae katika maisha.
Mrajisi wa elimu Zanzibar Siajabu Makame Pandu
“Lazima jamii iendelee kushirikiana na wizara ya elimu, katika kumaliza tatizo, na moja ni kiziripoti kesi hizo wanapogundua wazazi wamewaoza waume watoto wao’’,alisema
Afisa elimu na mafunzo ya amali wilaya ya Micheweni Mbwana Shaame, amesema huwenda kama malezi ya pamoja yakirudi na mtoto kulelewa na jamii, hali hiyo itapungua.
Mkuu wa Mkoa wa kaskazini Pemba Omar Khamis Othuman, amesema lazima jamii ifikirie mara mbili, umuhimu wa kumsomesha mtoto wa kike, bada ya kuunga mkono kwenye kumuozesha.
Mratibu wa FAWE Zanzibar, amesema moja ya sababu ya wazazi kuwaoza watoto wao, umaskini na hasa wa kumuendeleza mtoto bado ni changamoto.
Nae Mratibu wa mradi wa Kukuza Usawa wa kijinsia na Kuwawezesha Wanawake ‘GEWE’ kutoka Chama cha waandishi wa habari Tanzania TAMWA ofisi ya Zanzibar, Asha Abdi Makame, amesema mashine ya DNA pia ikiwepo inaweza kupunguza ubakaji  kwa watoto.             Haji Nassor, Pemba

0 comments:

Post a Comment