November 16, 2015


Kukosekana matumizi bora ya ardhi kumeiathiri  jamii kukosa uhalisia wa maeneo pamoja na mmong’onyonko wa ardhi kisiwani Pemba .
Mkurugenzi mtendaji wa asasi isiyo ya kiserikali ya Uhifadhi Misitu ya Jamii Pemba Mbarouk  Mussa Omar amesema hali hiyo imechangiwa na mtumizi mabaya rasilimali hasa zile zinazoizunguka jamii.
Amewashauri  wananchi  kisiwani humoa kufuata maelekezo ya  matumizi bora ya ardhi ili kuzuia athari zinazoendelea zinazosababishwa na mabadiliko ya tabia nchi.
Amefahamisha kuwa matumizi bora ya rasilimali hiyo ni pamoja na na kupanda miti katika maeneo ya wazi na kubadilika kuanza kutumia nisahti mbadala .
Afisa kilimo mseto wa asasi hiyo iliyopo huko Gando  Ali Hamad amesema kwa sasa wanahamasisha jamii kuanza kujihusisha na kilimo mseto kma njia ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi .

0 comments:

Post a Comment