Tume ya kurekebisha
sheria Zanzibar imesema imeshaandaa mkakati wa kuzifanyia marekebisho sheria mbali
mbali zenye mapungufu ili ziendane na mazingira ya sasa.
Mwenyekiti wa tume hiyo Jaji
Mshibe Ali Bakari
amesema mabadiliko katika sekta ya sheria yanalenga kuleta ufanisi na kutoa usimamizi bora.
amesema mabadiliko katika sekta ya sheria yanalenga kuleta ufanisi na kutoa usimamizi bora.
Amesema hatua hiyo
itafanikisha jamii kuwa na uelewa na utii wa sheria huku
ikirahisisha usimamizi wake.
Akifungua mafunzo ya
kupitia mkakati huo mjini Zanzibar amesema lengo ni kuweka maadili kwa
watendaji wakuu wa taasisi pamoja na kuwawezesha kusimamia
mabadiliko hayo.
Akitoa mada katika
mafunzo hayo Mhadhiri wa chuo Kikuu cha Mzumbe Dkt Julius Cosmas
amesema mfumo mbaya wa sheria na vitendo vya rushwa Zanzibar umechangia kukwama
kwa maendeleo katika sekta zote.
0 comments:
Post a Comment