November 19, 2015

Mwanasheria Mkuu wa serikali  ya Tanzania, George Masaju amepinga hoja  zilizoibuliwa na UKAWA kuhusu uhalali wa rais wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar, Dkt Shein, kuhudhuria kwenye uzinduzi wa Bunge.
Amesema kuwa tayari Tume ya uchaguzi ya Zanzibar ZEC imefuta uchaguzi, na kwa kuwa hakuna mtu yeyote alieapa kiapo cha urais tofauti na rais wa sasa wa Zanzibar, Dkt Shein.
 Hivyo Dkt Shein anatambulika kama rais wa Zanzibar na ana uhalali wote wa kuhudhuria katika uzinduzi wa Bunge la 11 huku akivitaja vifungu mbalimbali vya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977 na katiba ya Zanzibar 1984.
Masaju ametumia ibara ya 102 ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupangua hoja hizo inayoeleza kuwa, kutakuwa na serikali ya Zanzibar itakayo julikana kama serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itayokuwa na mamlaka katika Zanzibar juu ya mambo yote yasiyo mambo ya muungano kwa mujibu wa masharti ya katiba hii.


Pia ametumia katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 katika Ibara yake ya 26 ambayo inasema, kutakuwa na rais wa Zanzibar ambae atakuwa mkuu wa nchi ya Zanzibar, kiongozi wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi.

0 comments:

Post a Comment