November 24, 2015


Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF Maalim Seif Sharif Hamad na Kiongozi wa ACT- Wazalendo Bw. Zitto Kabwe, wameshiriki katika mazishi ya Marehemu Bi. Amina katika makaburi ya Mwanakwerekwe mjini Zanzibar.
Bi. Amina aliefariki ghafla jana (Jumatatu) aliwahi kuwa Mbunge wa Viti maalum CUF katika awamu iliyopita na baadaye alijiunga na Chama Cha ACT-Wazalendo.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF Maalim Seif Sharif Hamad, akitia mchanga katika kaburi la marehemu Bi. Amina Abdallah Amour katika makaburi ya Mwanakwerekwe Zanzibar. 
Kiongozi wa ACT- Wazalendo Bw. Zitto Kabwe, akitia mchanga katika kaburi la marehemu Bi. Amina Abdallah Amour katika makaburi ya Mwanakwerekwe Zanzibar wakati akishiriki mazishi hayo.
Viongozi mbali mbali wa CUF na kiongozi wa ACT Wazalendo Zitto Kabwe (wa tatu kushoto) pamoja na wananchi wakiitikia dua wakati wa mazishi ya marehemu Bi. Amina Abdallah Amour katika makaburi ya Mwanakwerekwe Zanzibar.

0 comments:

Post a Comment