Jumla ya wagonjwa 226 wa kipindupindu
wameripotiwa na kati ya hao watatu wamefariki tangu ulipobainika ugonjwa huo
mwezi sept mwaka huu katika shehia mbali mbali kisiwani Unguja.
Idadi hiyo inaelezewa
kuengezeka kutokana na wagonjwa wapya kuendelea kupokelewa na kupatiwa matibabu
katika kambi ya wagonjwa hao huko chumbuni nje kidogo ya mji wa Zanzibar.
Daktari dhamana wa kituo
hicho Ramadhan Mikidadi Suleiman amesema maeneo yaliyoathirika zaidi ni shehia Kinuni, Fuoni, Shaurimoyo na Kilimahewa.
Akitoa maelezo kwa Mkuu
wa mkoa wa mjini Magharib Abdallah Mwinyi Khamis alipotembelea katika kambi
hiyo daktari Mikidadi maeneo hayo yameathirika zaidi kutokana na wananchi kuendelea
kupuuza maelekezo ya wataalamu wa afya yakiwemo kuchemsha maji ya kunywa na
kufanya usafi wa mazingira wa maeneo yao.
Ameeleza kuwa jitihada
mbali mbali zimechukuliwa ikiwemo kutoa elimu ya afya kwa wananchi kupiga dawa
kwenye maeneo yaliyoathirika na kipindupindu pamoja na kutoa dawa za kulia
vidudu katika maji (water guard) kwa familia zilizoathirika na maradhi hayo.
Hata hivyo amefahamisha
kuwa kuna baadhi ya wananchi waliopatiwa dawa hizo wanazitumia kwa kufulia badala ya
kutia kwenye maji ya kunywa kama ilivyokusudiwa.
0 comments:
Post a Comment