Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli, amemuapisha Majaliwa Kassim Majaliwa kuwa
Waziri Mkuu wa Tanzania.
Majaliwa anakuwa waziri mkuu wa kumi na moja wa Tanzani ameapishwa baada ya Bunge kuthibitisha uteuzi wake hapo jana.
Hafla ya Kuapisha Majaliwa imefanyika kwenye Ikulu ya Chamwino mjini Dodoma na kuhudhuliwa na
viongozi mbalimbali wa serikali wakiwemo, Makamu wa Rais wa Tanzania, Samia
Hassan Suluhu, Rais wa Zanziba, Dk. Ali Mohammed Shein, Makamu wa Rais Mstaafu,
Dk. Gharib Bilal, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Job
Ndugai na Naibu Spika, Dk. Tulia Ackson, Wabunge, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na
Usalama, Jenerali Davis Mwamunyange na Wabunge.
Makamo wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa Kassim baada ya kuapishwa katika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma leo |
0 comments:
Post a Comment