Chama cha mapinduzi CCM kimesema ndoto za mchana Maalim Seif kuapishwa
kuwa Rais wa Zanzibar kwani Tume ya Uchaguzi Zanzibar tayari imeshatangaza
kufutwa kwa uchaguzi mkuu wa Zanzibar uliofanyika novemba 25 mwaka huu 2015.
Katibu wa Kamati Maalum ya NEC, CCM Zanzibar Waride Bakari
Jabu amesema mawazo hayo ya wana CUF ni kuwadanganya wananchi wakati wanafahamu
hali halisi ilivyo.
CCM pia imelaani kitendo cha wabunge
wa kambi ya upinzani wanaounda ukawa kuwazomea viongozi wakuu wa Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar wakati wakiingia katika ukumbi wa Bunge Dodoma.
Akizungumza na waandishi wa habari
katika ukumbi wa afisi kuu ya CCM Kiswandui Waride amesema kitendo hicho ni
ukosefu wa nidhamu.
Kwa kweli tabia ile si taba ya
kiungwana lakini pia walikusudia kuwavunjia heshima viongozi wakuu wa SMZ pamoja
na kuwasumbua wananchi kusikiliza hotuba ya rais wa jamburi ya Muungano wa Tanzania
Dkt John Magufuli alipolizindua bunge la 11” amesema Waride.
ameahamisha kuwa hayo sio matarajio
ya chama cha mapinduzi kilichoridhia mfumo wa vyama vingi vya siasa pamoja na
kuundwa kwa serikali ya Zanzibar yenye mfumo wa umoja wa kitaifa.
0 comments:
Post a Comment