November 14, 2015

Masheha wa shehia za Kojani Mkoa wa wa Kaskazini Pemba wametakiwa kuzuia ufanywaji wa biashara za majimaji ili kuzuia kuenea kwa ugonjwa wa kipindupindu.       Amri hiyo ameitolewa na Mkuu wa Mkoa huo Omar Khamis Othman alipotembelea kambi ya kipindupindu na kuelezea kusikitishwa na baadhi ya wananchi kuendelea kuuza biashara hizo   zilizopigwa marufuku.
Jumla ya wagonjwa 24 wa kipindupindu wamelazwa katika kambi hiyo tangu kuzuka kwa ugonjwa huo.
Amesema ni vyema kwa masheha na kamati  zao za afya kuhakikisha biashara za maji maji  haziuzwi hasa katika kipindi hiki cha mripuko wa ugonjwa wa kipindupindu.
Aidha Mkuu huyo wa Mkoa amewataka masheha kuondoa muhali katika kufanikisha agizo hilo  kwa kuwachukulia hatua za kisheria wanaokaidi kutekeleza agizo hilo. 
Kwa uapde wake Afisa wa afya kitengo cha magonjwa ya mripuko Said Khatib Juma amesema kuwa Wizara ya Afya kwa kushirikiana na masheha imeunda timu itakayofanya msako wa nyumba  zinauza juisi na malai ili kuzichukulia hatua.

0 comments:

Post a Comment