May 16, 2014

                                     
Watu watatu wamelazwa hospitali ya Mnazi mmoja kwa kuhofiwa kuathirika na ugonjwa wa Dengue baada ya kubainika kwa na dalili zake.
Akizungumza na waandishi wa habari Waziri wa afya Juma Duni Haji amesema    tayari vipimo vya wagonjwa hao vimepeleka Dar es salam  kwa uchunguzi zaidi   ili kupata uhakika  kama kweli ni ugonjwa huo.
Amesema ugonjwa huo unaoasababishwa na kirusi cha mbu mweupe (AEDES) anaetafuna mchana umegawika aina tofauti ikiwemo dengue ya homa, ya damu na ya kupoteza fahamu.            
Waziri duni ameongeza kuwa dalili kuu za dengue ni homa, kuumwa kichwa maumivu ya viungo na uchovu zinazojitokeza kati ya siku 3 na 14 au dalili zinazofanana na malaria.                      
Amesema mbu huyo huzaliana katika maji yaliyotuama hasa kwenye vyombo vya nyumbani, kingo za maji ya paa za nyumba, matairi ya gari, ndoo, vikopo na katika vifaa vidogo vidogo vinavyotuama maji na tayari wagonjwa kadha wamesharipotiwa jijini dar es salaam.
Waziri duni amewataka wananchi  kuwa waangalifu na kuchukuwa tahadhari ya kuhakikisha kuwa wanaondoa sehemu zote zinazoweza kuzalisha mbu ikiwemo madimbwi, vichaka na mashimo ya maji.                                                            
Nae Katibu mkuu Wizara ya afya Mohamed Saleh Jidawi  amesema ugonjwa wa Dengue hauna tiba wala chanjo na unatibiwa kutokana dalili zinazoambatana na ugonjwa huo ikiwemo kupungukiwa maji au damu.
Waziri wa Afya Zanzibar Juma Duni Haji akitoa tarifa kwa wandishi wa Habari juu ya kupatika kwa wagojwa watatu wa Homa mbaya ya (DENGUE) Visiwani hapa, na kuwataka wananchi kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo kuangamiza mazalio ya Mbu, kufyeka vichaka vilivyo karibu na makazi namengineyo ili kujinginga na kutafunwa na Mbu huyo.
 

0 comments:

Post a Comment