May 16, 2014

Jeshi la polisi linawashikilia wazazi wa mtoto wa Mussa Issa Say kwa tuhuma za kumjeruhi na pasi katika paja lake la mguu wa kushoto pamoja na kumuathiriwa jicho na kitu kisichojulikana.
Kamanda wa Mkoa wa mjini magharibi Mkadama Khamis Mkadama amesema mtoto huyo alifanyiwa ukatili huo  na baba yake mzazi Issa Mazaga Say kwa madai ya kuiba shilingi 200.
Akizungumza na waandishi wa habari   amesema tukio hilo limetokea tarehe kumi na tatu mwezi huu huko kilimahewa wilaya ya magharibi unguja.
Amesema jeshi hilo pia linamshikilia mama wa kambo wa mtoto huyo Khadija Jafar Rashid katika kituo cha polisi cha Ng’ambo kwa kuchochea vitendo hivyo vya ukatili kwa mtoto wao.
Kamanda Mkadam amesema kuwa tayari mtoto huyo ameshapelekwa hospitali Mnazi mmoja kwa matibabu na jeshi la polisi linaendelea kumpatia matibabu mengine zaidi .
Amewataka wazazi na walezi kuacha kuwapiga  watoto kwa hasira ili kuepusha madhara kwa watoto hao.

0 comments:

Post a Comment