April 25, 2014



Mkurugenzi Mipango, Sera na Utafiti
Wizara ya afya Zanzibar Abdullatif Haji.
 WIZARA ya Afya Zanzibar, imesema itahakikisha hatua zilizofikiwa za kupunguza vifo vya mama wajawazito na watoto wakato wa kujifungua zinakuwa endelevu ili kufikia malengo ya millennia.
Mkurugenzi Mipango, Sera na Utafiti katika wizara hiyo Abdullatif Haji, amesema katika mkutano wa siku moja kufunga mradi wa miaka mitano uitwao MAISHA uliofanyika katika hoteli ya Grand Palace Zanzibar, kuwa lazima juhudi za kuimarisha afya ya mama na mtoto ziendelezwe.
Mkurugenzi huyo amesema Zanzibar imepiga hatua imefanikiwa kupunguza vifo hivyo kutoka 377 mwaka 2012, hadi kufikia 221 kwa sasa.
Amesema serikali itaendeleza mkakati huo kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ukiwemo mradi wa MAISHA uliosaidia kupunguza vifo hivyo kwa asilimia 50 katika visiwa vya Unguja na Pemba.
“Lengo letu ni kuhakikisha hakuna mzazi anayekufa wakati wa kujifungua wala kupoteza kizazi chake,” amesisitiza.
Mkurugenzi huyo amesema mradi huo unaosimamiwa na taasisi ya Jhpiego Zanzibar chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani USAID, umesaidia kuwakomboa akinamama kwa kuwaelimisha juu ya umuhimu wa kujifungulia hospitali pamoja na kuhudhuria kliniki katika kipindi chote cha ujauzito.
Amefahamisha kuwa, vifo vya mama wajawazito na watoto vinaweza kupunguzwa na kumalizwa kabisa, kama kutakuwa na mkakati madhubuti wa utoaji huduma endelevu na uangalizi wa kutosha kabla na baada ya kujifungua.
Amesema lengo la Wizara ya Afya, ni kuhakikisha vya mama wajawazito vinavyotokana na uzazi pamoja na vya watoto wanaokufa wakati wa kuzaliwa, vinapngua hadi 150 ifikapo mwaka 2015.
Mapema, Mkurugenzi Mkazi wa Jhipiego nchini Tanzania Maryjane Lacoster, ameeleza kuwa mafaniko yaliyopatikana katika kuokoa maisha ya mama na watoto wakati wa kuzaliwa, yametokana na msaada na ushirikiano wa Serikali katika mpango huo wa miaka mitano, sambamba na ule wa taasisi nyengine nchini na zile za kimataifa.
Amesema mafanikio hayo yameipa moyo Jhipiego kuendelea kufanya kazi kwa karibu zaidi na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, sambamba na washirika wanaofadhili mpango huo katika kuhakikisha Wazanzibari wanakuwa na afya bora.
Naye Mwakilishi wa USAID nchini Tanzania Lisa Patel, ameishukuru Wizara ya Afya Zanzibar, kwa kuupa ushirikiano mradi huo uliorahisisha wanawake kupata huduma bora kutokana na vifaa vya kisasa wakati wa ujauzito, kabla na baada ya kujifungua.
Kwa upande wake, msimaizi mkuu wa mradi wa MAISHA Dk. Dunstan Bishanga, ameeleza kuwa, tangu kuanzishwa mradi huo mwaka 2008, zaidi ya watoa huduma 250 Unguja na Pemba, wamepatiwa mafunzo kuhusiana na jinsi ya kuwahudumia akina mama wajawazito na watoto

0 comments:

Post a Comment