April 25, 2014


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amesema wakati umefika kwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuanza kufikiria uwezekano wa kuanzisha chuo cha Uvuvi Zanzibar.

Dk. Shein amesema hayo katika mkutano wa kujadili Mpango kazi na bajeti ya mwaka 2013/14 ya Wizara hiyo kwa kipindi cha miezi tisa kuanzia mwezi Julai 2013.

Amesema mazingira ya Zanzibar pamoja na mahitaji ya ajira kwa vijana vinalazimisha kuweko kwa chuo maalum cha uvuvi kitakachosaidia kutoa mafunzo kwa wananchi wa Zanzibar wanaojihusisha na shughuli za uvuvi wakiwemo vijana.

Amezisisitiza taasisi za umma zikazingatia thamani halisi ya bei ya bidhaa na huduma zitakazohitajika wakati wa kupanga na kutekeleza majukumu ya taasisi zao ili kuwa na bajeti halisi kwa mahitaji halisi.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dk. Kassim Gharib Juma amesema Wizara amesema kumekuwa na mafanikio makubwa katika udhibiti wa maradhi yasiyo na mipaka pamoja na maradhi ya kichaa cha mbwa kutokana na kuimarika kwa huduma za chanjo.

aidha ameeleza pia sekta ya uvuvi imekuwa na ongezeko la wavuvi wa baharini ambapo katika  kipindi cha mwaka wa fedha 2013 – 2014 jumla ya tani 23,000 za samaki zilivuliwa na zimewaingizia wavuvi jumla ya shilingi bilioni 89.7.

0 comments:

Post a Comment