April 27, 2014

Vijana wengi Zanzibar wanashindwa kutumia fursa za ajira zilizopo kutokana na  ukosefu wa taaluma na uwezo wa kuzifia fursa hizo.
Afisa kutoka Wizara ya ustawi wa jamii maendeleo ya wanawake na watoto Zanzibar   Zeyana  Ahmed Kassim  amesema  ajira hizo zinapatikana katika sekta ya uvuvi, utalii, kilimo, biashara na elimu na bado hawajapewa kipaumbele na kundi hilo.
Amewataka vijana kufanya utafiti wa makini juu ya fursa hizo ili kuondokana na utegemezi wa ajira kutoka serikalini.
Zeyana alikuwa akizungumza katika jukwaa la majadiliano yaliyolenga kuimarisha mawasiliano baina ya vijana na Serikali katika kuzifikia ajira Mjini Zanzibar.
Nao vijana hao wameiomba serikali kubadili mfumo wa kuendelea kuwarudisha wastaafu kazini inawanyima fursa vijana  nafasi hizo. 

0 comments:

Post a Comment