Serikali ya Jamuhuri ya Watu wa China imekukubali
kugharamia ujenzi wa Kiwanja cha michezo cha Mau Tse Tung kilichopo miperani
Kikwajuni Mjini Zanzibar.
Kauli hiyo imetolewa na Balozi Mdogo wa Jamuhuri ya Watu wa China aliyepo Zanzibar Bw. Xie Yunliang wakati akizungumza na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi huko Mjini Dodoma.
Kauli hiyo imetolewa na Balozi Mdogo wa Jamuhuri ya Watu wa China aliyepo Zanzibar Bw. Xie Yunliang wakati akizungumza na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi huko Mjini Dodoma.
Balozi Xie Junliang alimueleza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwamba
Timu ya wataalamu wa China inatarajiwa kukifanyia utafiti na uchunguzi kiwanja
hicho baadaye mwaka huu sambamba na utiwaji saini Makubaliano ya ujenzi wa
kiwanja hicho unaotarajiwa kufanyika mapema mwaka ujao.
Alisema ujenzi wa uwanja huo uliopewa heshima ya Jina la Kiongozi
muasisi wa Taifa la China Marehemu Mao Tse Tung utajumuisha kiwanja cha mchezo
wa soka pamoja na michezo mengine ya ndani kama vile Table Tennis.
“ Tunatarajia ujeni wa kiwanja cha Mao utakapokamilika utakuwa na uwezo
wa kuhudumia wanamichezo wa michezo tofauti ukiwemo ule unaopendwa zaidi wa
soka “. Alisema Bwana Xie Junliang.
Alimuhakikishia Balozi Seif
kwamba Jamuhuri ya Watu wa China itaendelea kuiunga mkono Zanzibar na Tanzania
kwa ujumla katika harakati zake za kujikwamua kiuchumi.
Akitoa shukrani zake Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ameipongeza Jamuhuri ya Watu wa China kwa moyo wake wa kuendelea kuiunga mkono Zanzibar na Tanzania kwa ujumla katika miradi ya Kiuchumi na Maendeleo.
Akitoa shukrani zake Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ameipongeza Jamuhuri ya Watu wa China kwa moyo wake wa kuendelea kuiunga mkono Zanzibar na Tanzania kwa ujumla katika miradi ya Kiuchumi na Maendeleo.
Alisema mchango wa Serikali ya
China kwa Zanzibar umesaidia kuiwawezesha asilimia kubwa ya Jamii Zanzibar
kustawika Kijamii na hata kiuchumi kupitia miundo mbinu iliyowekwa na Serikali
kwa msaada wa Nchi hiyo rafiki.
0 comments:
Post a Comment