Umoja wa Mataifa
umeikosoa serikali ya Myanmar kwa kukiuka ahadi ilizotoa kwa kuwazuia Waislamu wa nchi hiyo kushiriki
kwenye sensa ya idadi ya watu.
Mfuko wa Sensa ya Jamii wa Umoja wa Mataifa
(UNFPA) umesema Myanmar iliahidi kuheshimu na kuzingatia viwango vya kimataifa
na misingi ya kisheria katika zoezi hilo.
Limeeleza kuwa
kutokana na vizuizi vilivyowekwa kwa Waislamu wa kabila la Rohingya inanaitilia
shaka sensa hiyo na inaweza kasababisha
kuongezeka mivutano katika mkoa wa Rakhin.
Sensa hiyo ya watu
ni ya kwanza kufanyika nchini Myanmar katika kipindi cha miongo mitatu
iliyopita, imeanza Jumapili iliyopita na itaendelea hadi April 10.
Serikali ya Myanmar haiwatambui rasmi Waislamu
wa nchi hiyo na hawasaidi na mashambulizi ya umwagaji damu yanayofanywa
dhidi yao na Mabudha wa nchi hiyo wenye misimamo mikali.
0 comments:
Post a Comment