Mfanyakazi
mmoja wa kike katika Hoteli ya MELIA iliyopo Kiwengwa Mkoa wa Kaskazini Unguja
amedai kubakwa na mfanyakazi mwenziwe hotelini hapo.
Akizungumza na vyombo vya habari
kwa masikitiko Neema mwenye umri wa miaka 25 amesema amefanyiwa udhalilishaji huo
februari 18 na Nicolas Msambi ambae ni mfanyakazi wa kitengo cha ulinzi katika
hoteli hiyo.
“…Ilikuwa majira ya jioni niliombwa
na meneja wa ulinzi wa hoteli ya melia kumpika chakula nyumbani kwake
hotelini humo lakini baadae aliniachana Nicolas ambae alinivamia
kwa nguvu.” Neema ameeleza.
Uchunguzi umebaini pia mwanamke huyo ameombwa
kulipwa fidia ya shilingi milioni mbili kufuta kesi hiyo iliyotokea siku chache
baada ya mfanyakazi mwengine wa hoteli ya Melia jina linahifadhiwa kudai
kuvuliwa nguo mbele ya wafanyakazi wa kiume kwa madai ya kuiba Dola mbili
katika chumba cha mgeni.
Uongozi wa hoteli hiyo umekataa
kuelezea juu ya tukio hilo huku kwa waandishi wa habari waliofuatilia tukio
hilo.
Jeshi la polisi mkoa wa
kaskazini unguja limethibitsha tukio hilo na kueleza linaendelea na
upelelezi wa madai ya kubakwa mfanyakazi huyo wa kampuni ya ulinzi ya
security group.
Akielezea tukio hilo Kaimu
Kamanda wa polisi Mkoa huo Salma Khamis amefahamisha kuwa wamekusanya sampuli
za mtuhumiwa ili kuchunguza vinasaba jijini Dar es salaammanamke abakwa
kwa upande wake katibu mtendaji
wa kamisheni ya utalii amesema tukio hilo linashughulikiwa na Kamisheni ya kazi
Zanzibar ambayo pia imesema haihusiki na kesi za aina hiyo
“…….Sisi hatuhusiki na
kesi kama hizo kwa mujibu wa sheria ya kazi Zanzibar tunasimamia migogoro
na malamimiko ya wafanyakazi kesi hizo zinashughulikiwa na polisi
alifafanua kamishna wa kamishemni ya kazi Zanzibar.
0 comments:
Post a Comment