November 24, 2015


Chama cha siasa cha wakulima Tanzania AFP kimelaani kitendo kilichofanywa na wabunge wa upinzani chini ya mwavuli wa UKAWA kuwazomea viongozi wa Zanzibar jambo walilodai  limelitia aibu taifa.
AFP kimesema kitendo hicho hakifai kufumbiwa macho na badala yake kinapaswa kupingwa ikizingatiwa wabunge hao wamefanya hilo katika chombo cha kutunga sheria.
Mwenyekiti wa chama hicho taifa Said Soud Saidi amesema inashangaza kuona viongozi waliochaguliwa na wananchi kuwawakilisha katika bunge hilo wanafanya mambo yasiyokuwa na maana.
Amemuomba spika kuwachukulia hatua za kisheria wabunge waliofanya kitendo hicho kwani pia  kimelipa sifa mbaya bunge hivyo.
 Aidha mwenyekiti huyo wa AFP ameipongeza hutuba ya rais wa Tanzania Dkt  John Magufuli aliyoitoa alipokuwa akifungua bunge la 11 kwa kuonesha  muelekeo mzuri wa uongozi wake unakwenda sambamba na kauli yake ya hapa kazi tu.

0 comments:

Post a Comment