May 07, 2014

 Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe Balozi Seif Alli Iddi anafunga mkutano Mkuu wa 12 wa Chama cha Majaji Wanawake Tanzania (TAWJA) kwa kushirikiana na Chama cha Majaji Wanawake Duniani (IAWJ) Arusha, Tanzania.
Majaji Wanawake takribani 600 kutoka nchi mbalimbali duniani wakiongozwa na Jaji wa Rufaa (Mstaafu), Rais Eusebia Munuo, wa tanzania ulifunguliwa na Rais wa Tanzania tarehe 05 Mei, 2014 .
Mkutano huo unajadili mada ni Haki kwa wote, kupanua wigo wa mawasiliano kati ya Majaji Wanawake duniani ili kujenga mazingira mazuri ya utendaji kazi pamoja na kujenga ubora na uadilifu katika utoaji haki na ukuzaji (promotion) wa Haki za Binadamu.
 Chama cha Majaji Wanawake Duniani (IAWJ) kilichoshirikiana na (TAWJA) kiliundwa rasmi mwaka 1991 na kina wanachama takribani 4,000 kutoka kiasi ya nchi 100 kutoka katika kila ngazi ya Mahakama.

Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa katika
picha ya pamoja na baadhi ya Washiriki wa Mkutano wa Majaji Wanawake Duniani,
Mara baada ya kufungua mkutano huo

0 comments:

Post a Comment