April 14, 2014

zenjkiwe.blogspot.com
Asha Abdi Afisa utetezi TAMWA
Zanzibar
Jamii imetakiwa kutokuwaonea huruma wanafanya vitendo vya ubakaji badala yake kuwafikisha katika vyombo vya sheria ili kuchukuliwa hatua kali dhidi yao.
Afisa utetezi wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) Zanzibar Asha Abdi amesema vitendo hivyo havipaswi kunyamzaiwa kwa vile vinaweza kumuathiri alifanyiwa kitendo hicho kiafya na kiakili hata ni kinyume na haki za msingi.
Ametoa kauli hiyo kufuatia matokeo ya hivi karibuni ya ubakaji yaliyoripotiwa kutoka Mkoa wa Kaskazini Unguja likiwemo la kubakwa kwa mfanyakazi wa hoteli ya kitalii ya Melia, la mtoto wa miaka 12 huko Mahonda pamoja na lile la kumwagiwa maji ya moto mfanyakazi wa ndani huko Kwamtipura, Wilaya ya Mjini.
Afisa Asha amesema kesi ya ubakaji katika hoteli ya Melia ambayo mtuhumiwa ni Mkuu wa kitengo cha ulinzi katika hoteli hiyo amemuomba radhi mhusika kufuatia kesi hiyo kuripotiwa polisi.
Tamwa imetoa pole kwa wahusika wote walofikwa na matukio ya ukatili na kuiomba Serikali kuweka utaratibu mzuri wa kuchukuliwa hatua za washukiwa ili kukomesha vitendo hivyo.  

 

0 comments:

Post a Comment