April 14, 2014


Taasisi za Serikali na zisizo za kiserikali Pemba zimetakiwa kushirikiana katika kuwaelimisha wananchi athari za mabadiliko ya tabia nchi zilizoanza kuithiri Zanzibar.

Afisa Mazingira wa kitengo cha kukabiliana na madiliko tabia nchi Salum Hamad Bakar amesema ushirikiano huo ni muhimu katika kusaidia wananchi kufahamu athari za mabadiliko hayo yanapotokea.

Akizungumza katika majailiano ya kuwasilisha makakati wa mawasiliano kuhusu mabadiliko ya tabia nchi Zanzibar kwa viongozi wa taasisi mbali mbali kisiwani Pemba amefahamisha kuwa maeneo kadhaa ya kilimo na kiuchumi katika ukanda wa pwani yameathirika na mabadiliko hayo hivyo juhudi zaidi zinahitajika kusambaza uelewa kwa jamii.

Zaidi ya maeneo 160 ya zanzibar yameripotiwa kuvamiwa na maji ya bahari kutokana na kuongeza kina chake kulikochangiwa na athari za mabadiliko hayo.

Akiwasilisha maada hiyo Ruzika Niyo Muheto amesema sera ya mazingira imeainisha maeneo mbali mbali yaliyovamiwa na maji ya chumvi hali inayotilia shaka hatma ya maisha yao na kusisitiza umuhimu wa sekta zote za Serikali na Binafsi kutekeleza mkakati huo kwa maslahi ya taifa.

Nae Afisa Idara ya kilimo Pemba Idrisa Hassan Abdalla ameitaka kuelezwa kwa kina sababu zinazopeleka suala la mabadiliko ya tabia ya nchi ili wananchi wafahamu athari zake na kuchukuwa hatua.

0 comments:

Post a Comment