April 13, 2014

Waislamu mbalimbali nchini wametakiwa kutoa michango yao ili kufanikisha ijitimai ya kimataifa inayotarajiwa kuanza juni 16 mwaka huu.
 Ijitimai hiyo inafanyika kila mwaka kwa karibu miaka 20 sasa ikiwa na lengo la kuwakumbusha waumini wa dini  hiyo juu ya mambo mema.
Naibu wa jumuiya ya Fiisabillahi Tablighi Markaz Zanzibar Sheikh Wakati Hassan amesema tayari maandalizi yameanza kwa ajili ya ijitimai hiyo ikiwemo ujenzi wa baadhi ya sehemu mbali ikiwemo vyumba na vyoo.
 Amefahamisha kuwa ijitimai hiyo itahudhuriwa na waislamu kutoka nchi za Uganda, Afrika ya kusini, Malawi, Zambia, Kenya, Rwanda na Tanzania bara.

0 comments:

Post a Comment