April 13, 2014

zenjkijiwe.blogspot.com
Kamishna wa Elimu
Zanzibar
Maryam Abdalla Yussuf
Kamishna wa Elimu Zanzibar Maryam Abdalla Yussuf amesisitiza kuwekwa nguvu zaidi za  kuwahamasisha wanafunzi walioacha masomo kufahamu uhumhimu wa elimu na kurejea skuli za msingi na sekondari.
Amesema utafiti wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya  Amali Zanzibar umegundua  sababu mbali mbali zinazochangia wanafunzi kutoroka skuli ikiwemo tabia ya baadhi ya wazazi kutowapatia mahitaji muhimu ya kimasomo watoto wao.
Akizungumza katika uzinduzi wa mradi wa kuhamasisha kupunguza wimbi la utoro maskulini wa jumuiya ya kuwanasua vijana na watoto katika matatizo yanayowakabili (zao) Kamishna Maryam amesema iwapo umuhimu wa elimu utahamasishwa zaidi kwa wanafunzi utapunguza tatizo hilo la utoro.
Amefahamisha tabia ya vijana kuacha masomo kunaongeza idadi ya watoto wasiojua kusoma na kuandika kunapunguza idadi ya wasomi wanaohitajika kwa maendeleo ya Zanzibar.

zenjkijiwe.blogspot.com
wanafunzi zanzibar
Amewataka walimu na wazazi kufuatilia kwa karibu maendeleo ya watoto wao kwani nimiongoni mwa jukumu lao  muhimu katika kuwandaa kimasomo watoto wao.
Fatma Bakari Makame akisoma risala amesema   jumuiya hiyo imelenga kuelimisha vijana juu ya athari za maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa wanafunzi pamoja na kupiga vita mimba za umri mdogo na imefanikiwa kuwarudisha wanafunzi  kuendelea na masomo katika skuli za Mtopepo A, Kilimahewa, Mwembe Makumbi na wengine wamepelekwa katika Kituo cha Elimu mbadala.

 

 



  

0 comments:

Post a Comment