April 13, 2014

 
Makamu wa Rais wa Tanzania Dr. Mohamed Gharib Bilal na Waziri wa Miundombinu Dk. John Magufuli,Kamanda wa polisi Kanda maalum ya Daresalaam Suleiman Kova, Mkuu wa mkoa huo Said Mecky Sadick wamenusurika katika ajali ya Helkopta wakati akikagua uharibifu wa miundombinu uliosababishwa na mvua kubwa  katika jiji hilo.
Viongozi hao akiwemo mpiga picha wa Shirika la Utangazaji la TBC, George Kasembe wamepatiwa matibabu kwa majeraha waliyoyapata na wameendelea na ziara yao  ya kuangalia athari za mvua..
Kiasi ya  watu 10 wakiwemo watoto wadogo wameripotiwa kupoteza maisha kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha katika jiji la dar es salaam pamoja na kusababisha uharibifu mkubwa wa mali na miundombinu ya  madaraja na nyumba za makaazi.
Kamanda wa kanda maalum  Dar es salaam Suleiman Kova mapema aliarifu kuwa hali sio nzuri   jijini humo   na  kuwataka wananchi kuchukuwa  tahadhari kwenye makazi yao na kupunguza mizunguko isiyo ya lazima kutokana na   njia  nyingi kuwa  na mashimo.


 

 

0 comments:

Post a Comment