Amesema
matokeo ya utafiti huo yamekuwa msingi wa kuandaa Sera ya Maendeleo ya Watu hao Zanzibar.
Katika
kikao hicho cha kujadili wa Taarifa ya Utekelezaji wa Mpangokazi wa Ofisi ya
Makamu wa Kwanza wa Rais kwa kipindi cha robo tatu ya mwaka wa fedha 2013/2014 rais
Shein amehimiza suala la vipaumbele vya Wizara na Idara kwenda sambamba na
majukumu ya msingi ya Wizara na Idara (core functions) husika.
Kuhusu
suala la msaada wa uendeshaji wa vituo vya vijana walioacha madawa ya kulevya
nchini maarufu ‘Sober Houses’ amehimiza ushiriki wa wadau wengi zaidi na
Ofisi hiyo kuangalia kwa upana zaidi suala hilo ikiwemo kuandaa mpango maalum endelevu wa msaada wa jamii na Serikali kwa vituo
hivyo.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Bi Fatma Abdulhabib Fereji amesema kipindi cha Julai 2013 hadi Machi 2014 afisi
hiyo imekamilisha utafiti huo Mkakati wa Taifa wa Mabadiliko ya Tabianchi.
Amesema
katika mwaka ujao wa fedha ni Sera ya Maendeleo ya Watu wenye Ulemavu, Sera ya
UKIMWI, Kanuni ya Sheria ya Dawa za Kulevya, Mkakati wa Kudhibiti Taka Ngumu na
Mpango wa Utekelezaji wa Mabadiliko ya Tabianchi.
0 comments:
Post a Comment