Amesema
licha ya kupiga hatua katika sekta hiyo idadi ya raia wa nchi hiyo hasa katika utalii wa daraja la kwanza ni kiwango kidogo ikilinganishwa
na wageni wanaotembelea Zanzibar.
Alikuwa akizungumza na ujumbe wa Shirika la
utangazaji la Marekani (VOA) ukiongozwa na mtangazaji Dk Shaka Salli unaoangalia
namna Zanzibar ilivyofaidika katika miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Waziri Mbarouk amemshauri mtangazaji huyo kusaidia
kutangaza na kushawishi raia wa nchi hiyo kutembelea Zanzibar na Afrika.
Aidha
ameliomba shirika la VOA kujenga ushirikiano na Shirika la utangazaji la Zanzibar
ZBC kwa ajili ya kuwapatia mafunzo waandishi wa habari ili kuimarisha ufanisi
wa kazi zao.
Nae Dk Shaka Salli
amesema voa iko tayari kushirikiana na zbc katika kukuza matangazo yake na
sekta ya utangazaji Zanzibar
0 comments:
Post a Comment