Jumla ya vyandarua 780,000 vinatarajiwa kugaiwa
kwa wananchi wa wilaya zote za Zanzibar na Kitengo cha kumaliza malaria Zanzibar.
Ugawaji wa vyandarua hivyo utaanza March 16, 2016
utaanzia katika wilaya nne ikiwemo ya Magharibi A na B, Mjini na ya Mkoani
Pemb.
kazi kama hiyo ya ugawaji wa vyandarua majumbani
kwa mara ya mwisho ilifanyika mwaka 2012.
Akizungumza na waandishi wa habari Mjini Zanzibar kuhusu shughuli hiyo Mkuu wa sehemu ya
uhamasishaji wa kitengo hicho Mwinyi Issa Khamis amesema wameamua kuanza katika
shehia hiyo kutokana na kugundulika kuongezeka maabukizi ya malaria.
Kitengo hicho pia kimeanza upigaji dawa
majumbani ambapo kiasi ya nyumba 26,336 katika shehia 45 za Zanzibar itapigwa dawa hiyo.
Mkuu wa kazi za upigaji dawa mbu wa malariar Rashid
Abdalla amesema mpango huo unalenga kufikia asilimi 85 ya idadi hiyo ili
kuhakikisha wanapunguza wingi wagonjwa Zanzibar.
Amesema kwa sasa shughuli hiyo imerahisishwa
zaidi na kupelekwa kwa wananchi ambapo kumewekwa vituo maalum vya utoaji huduma
kwa haraka.
Mapema akitoa maalezo kwa waandishi wa
habari Kaimu Meneja wa kitengo cha Kumaliza Malaria Zanzibar Mwinyi Issa Mselem amesema kazi hizo ni
katika kukabiliana na ugonjwa huo.
Amesema wameamua kufanya mikakati hiyo kwa
kuzingatia kuwa kuzingatia kipindi cha mvua ambacho ni cha maambukizi mengi
kinakaribia.
Amewaomba wananchi kuvitumia vyandarua
watakavyogaiwa pamoja na kukubali kupigiwa dawa za kuulia mbu wa malaria katika
vyumba yao.
0 comments:
Post a Comment