Watu wasiojulikana usiku wa kuamkia leo wamechoma moto nyumba
saba pamoja na kituo cha Afya cha kiuyu Minungwini katika Mkoa wa
Kaskazini Pemba.
Matukio hayo yametokea
majira ya saa nane usiku yamehusisha nyumba mbili katika shehia ya Kangagani, nyumba mbili micheweni na moja katika
kijiji cha Gando.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskaziuni Pemba Hassan Nassir Ali amesema
uchunguzi wa awali umebaini kuwa nyumba hizo zimechomwa moto kwa kutumia mafuta
ya taa.
Ameongeza kuwa hakuna mtu aliejeruhiwa katika matukio hayo na jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi kuwabaini waliofanya tukio hilo ili kuwafikisha ktika vyombo vya sheria..
Ameongeza kuwa hakuna mtu aliejeruhiwa katika matukio hayo na jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi kuwabaini waliofanya tukio hilo ili kuwafikisha ktika vyombo vya sheria..
Amewataka wananchi kuendelea kuwa watulivu huku jeshi la Polisi
likiimarisha ulinzi.
Mmoja wa wananchi walichomewa nyumba yao Hadia Faki Ali wa kijiji cha Kangagani amesema
yeye na watoto wake saba walikuwa wamelala na wameshtushwa baada kuongezeka
joto kali ndani ya nyumba yao walipotoka nje
walibaini kuwa nyumba yao inaungua.
Hata anashkuru kwa kuwa wote walitoka salama hakuna aloungua
ingawaje vitu vyao vyote vimeteketea kwa moto huo.
Wakati huo huo kufuati kujitokeza kwa matukio hayo Mkuu wa Mkoa wa
Kaskazini Pemba Mh, Omar Khamis Othman amepiga marufuku mikusanyiko ya vikundi katika
maeneo mbali mbali kuanzia saa mbili za usiku.
Matukio ya uchomaji wa moto nyumba za wananchi na maskanii za vyama vya siasa yamekuwa yakishamiri hivi sasa kisiwani Pemba na sababu kubwa inadaiwa kuwa ni masula ya kisiasa.
Matukio ya uchomaji wa moto nyumba za wananchi na maskanii za vyama vya siasa yamekuwa yakishamiri hivi sasa kisiwani Pemba na sababu kubwa inadaiwa kuwa ni masula ya kisiasa.
0 comments:
Post a Comment