December 04, 2015


Uwanja wa pemba unatarajiwa kuanza kutoa huduma za kuruka na kutua ndege nyakati zote  hivi karibuni
Hii ni kufuatia kukamilika mradi wa uwekaji taa katika njia za kupitia ndege uliogarimu kiasi cha shilingi bilioni 1.5
Fundi wa Mamlaka ya viwanja vya ndege Zanzibar Mzee Abdalla amesema  uwanja huo kwa sasa utakuwa na uwezo wa kutoa huduma hadi usiku na mchana tofauti na ilivyokuwa awali zinaishia saa kumi na mbili za jioni.
Amesema tayari  majaribio ya awali ya taa hizo yamefanyika na sasa wanaendelea na kazi za kubadilisha miundo mbinu ya mfumo wa umeme na kuweka wa kisasa uwanjani hapo.
Funfi Aballa amefahamisha kuwa mfumo huo utaweka mtandao wa pamoja wa umeme ambapo pia wataweka jenereta litakalosadia kuendelea na kazi inapotokea hitilafu ya umeme.
Uwakaji wa taa hizo unafanyikwa chini ya kampuni moja kutoka Ujerumani ya Sage Gate awali ulitarajiwa kumalizika mwezi Septemba mwaka huu.

0 comments:

Post a Comment