Mkoa wa Mjini Magharibi bado unakabiliwa na ongezeko
la wagonjwa wa kipindupindu wanaoripotiwa
katika katika kambi ya wagonjwa hao iliyopo hospitali ya Chumbuni nje kidogo ya
mji wa Zanzibar.
Taarifa zinazema hadi sasa wagonjwa 30 wanaendelea
kupatiwa matibabu idadi iliyofikisha watu 342 walioambukizwa
kipindupindu huku 7 kati yao wamefariki dunia tangu kuibuka ugonjwa huo mwezi Septemba
mwaka huu.
Daktari dhamana kanda ya Unguja Fadhil Mohamed
Abdullah amesema asilimia 91 ya wagonjwa hao wanatoka katika shehia za Wilaya ya
Magharibi na shehia zilizoathirika zaidi ni Kiembesamaki, Mbweni, Kinuni,
Kihinani, Fuoni na Tomondo.
Amewaambia wiongozi wa Mkoa mjini
magharibi na maafisa afya kuwa tafiti za wataalamu wa afya zimebaini asilimia
80 ya maradhi hayo yamesababishwa na wananchi kutumia maji ya kunywa yasiyo
salama na vyakula vya majimaji vilivyoathiriwa na vimelea vya kipindupindu.
Ameomba mkoa huo kuwa na mikakati ya pamoja katika
kukabiliana na mripuko wa maradhi ya kipindupindu hasa kwa kutolewa elimu zaidi
kwa wananchi kuchemsha maji ya kunywa na kutia dawa maji ili kuyatokomeza kabisa.
Nao uongozi wa Mkoa Mjini Magharibi umeahidi
kuiendeleza mikakati ya kukabiliana na maradhi hayo kwa kushirikiana na
masheha na kuangalia uwezekano wa kupiga
marufuku uuzwaji wa vyakula vya majimaji iwapo wananchi watendelea na kupuuza maelekezo
yayotolewa na wataalamu wa afya.
0 comments:
Post a Comment