November 13, 2015

Aliyekuwa Spika wa Bunge la Kumi, Anne Makinda amesema hatagombea tena nafasi ya Uspika wa Bunge la 11 la tanzania.
Mama Makinda amesema kuwa hanampango wa kugombea tena nafasi hiyo na wala hajachukua fomu kama inavyo elezwa na baadhi ya watu.
Hata hivyo, hadi pazia la kuchukua na kurudisha fomu za kuwania Uspika wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linafungwa, Mama Anna Makinda alikuwa hajarudisha fomu yake hivyo kuonesha dhahiri kuwa ameachana na mpango huo.
Aliyekuwa Spika wa Bunge la Kumi, la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Anne Makinda ametangaza kutogombea nafasi ya Uspika wa Bunge baada ya kuliongoza Bunge hilo kwa kipindi cha miaka mitano.
akizingumza na waandishi wa habari katika ofisi za Bunge jijini Dar es Salaam Makinda amesema ameona wakati umewadia wa kuwaachia wengine kusika wadhifa huo katika  Mhimili huo muhimu wa Serikali.
Ameongeza kuwa ametumikia nafasi mbalimbali katika Siasa kwa kipindi cha miaka 40 ndani ya Bunge, ikiwemo nafasi ya Waziri ,Mwenyekiti wa Bunge,Naibu Spika na Spika  hivyo  kwa sasa ameamua kung’atuka katika masuala ya uongozi.
 “Kama yalivyo matakwa ya kisheria na demokrasia ya hapa nchini wanasiasa wanatumikia nafasi zao mbalimbali kwa kipindi cha miaka mitano na kisha wanarudi kuomba tena ridhaa kwa wananchi kuongoza”,alisema Mhe.Makinda.
Hata hivyo Mheshimiwa Spika amewaambia waandishi wa habari kuwa katika kipindi cha uongozi wake, Bunge lilifanyakazi kwa ushirikiano na liliweza kuisimamia Serikali hadi kupelekea baadhi ya Mawaziri kujiuzulu.
Ameongeza kuwa Bunge la 10 lilifanikiwa kubadilisha mfumo wa bajeti kwa kuweka sheria mpya za bajeti ambayo iliongeza nidhamu katika matumizi ya fedha.
Teyari Makada 21 wa CCM wamejitokeza kuwania nafasi ya Uspika wa Bunge akiwemo Dkt. Emmanuel Nchimbi, Samwel Sitta, Dkt Didas Masaburi, Balozi Philip Marmo, , Job Ndugai, Abdallah Mwinyi na Mussa Hassan ‘Zungu’ anaewania unaibu spika ni miongoni mwa majina ya makada wa CCM waliojitokeza kuwania nafasi hiyo.
Spika wa bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mh. Anna Makinda katikati akiwa katika picha ya pamoja na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza mkutano wake katika ofisi za bunge leo jijini Dar es salaam.(MAELEZO-Dar es salaam).

0 comments:

Post a Comment