Jaji mkuu wa Zanzibar Omar
Othman Makungu amewataka wanasheria kuingia katika ushindani wa kibiashara na
uwekezaji wa fani hiyo huku wakizingatia kuendelea kutoa huduma bora za
kisheria kwa wananchi wa kipato cha chini.
Amesema mabadiliko hayo ya kitaaluma iwapo yatazingazitia
hali halisi ya wananchi wa kipato cha chini na kwa kutumia wanasheria wazalendo
badala ya wageni kwa lengo la kuongeza kipato cha nchi.
Rai hiyo ameitoa wakati
akifungua mkutano mkuu wa Jumuiya ya wanasheria mawakili wan chi za Afiraka
Mashariki uliofanyika katika Hoteli ya Sea Cliff huko Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Amewashauri kuweka msisitizo
wa kukemea tabia ya wawekezaji wa kimataifa wanaofungua makampuni makubwa ya
kibiashara katika nchi za Afrika Mashariki wanao watumia wanasheria kutoka nchi
za kigeni na kuwakosesha fursa wanasheria wazalendo wenye uzoefu huo.
Nae Rais wa Jumuiya ya
wanasheria mawakili ya Afrika Mashariki, Nassor Khamis Mohamed amesema mkutano
huo licha ya kujadili suala la uwekezaji kupitia fani ya sheria pia watajadili namna
ya kuweka mazingira ya nchi za Afrika Mashariki ikiwemo Tanzania Bara,
Zanzibar, Kenya, Rwanda, Burudi, Rwanda, Uganda zinaendelea kuwa salama kwa msaada wa kisheria.
Baadhi ya Washiriki kutoka
sehemu mbalimbali wakifuatilia mkutano huo.
|
Baadhi ya Washiriki wa
Mkutano huo wa Kimataifa wa 20 wa Wanasheria wa Afrika Mashariki wakiwa katika
Ukumbi wa Mkutano.
|
0 comments:
Post a Comment