
Wagonjwa hao wameripotiwa katika vituo vya afya mbali mbali ikiwemo Kidongo chekundu, Kivunge, Pwani mchangani na hospitali ya Makunduchi pekee iliyopo Wilaya ya Kusini Unguja imepokea wagonjwa 2498
Mratibu wa afya ya akili zanzibar Dk Suleiman Abdu Ali amewaambia waandishi wa habari kuwa ingawa sababu ya matatizo hayo haijafahamika lakini wengi wao wanachangiwa na matumizi ya dawa za kulevya, urithi, na msongo wa mwazo na wasiwasi.

Muuguzi wa wagonjwa katika hospitali ya wagonjwa wa akili ya kidongo chekundu Bai Kumvi Juma amewaomba wazazi kuwa tayari kutoa misaada kwa wagonjwa hao ili kuwalinda na matatizo ya kijamii
Siku ya afya ya akili duniani huadhimishwa kila ifikapo October 10, na kauli mbiu ya mwaka huu ni JAMII IISHI NA WAGONJWA WENYE MATATIZO MAKUBWA YA AKILI.
0 comments:
Post a Comment