April 29, 2014


Hospitali ya Mnazi mmoja inakabiliwa na ukosefu wa sehemu ya kutoa matibabu ya magonjwa ya macho hali inayokwamisha utoaji wa huduma hizo kwa ufanisi kwa wananchi.

Katibu wa hospitali hiyo Hassan Makame Mcha amesema jengo walilokuwa wakitumia kutoa huduma hiyo limeshindikana kuendelea kutumiwa licha ya kufanyiwa matengenezo mara mbili.

Amefahamisha kuwa wafadhili wamejitokeza kulijenga upya jengo hilo ili kutoa tiba za macho kulingana na teknolojia za kisasa lakini mamlaka ya Mji mkongwe imekataa ujenzi wowote ulio kinyume na asili ya jengo hilo.

Katibu huyo  ameiomba serikali kusaidia juhudi za kufanikisha upatikanaji wa jengo la matibabu hayo katika hospitali ya mnazi mmoja ili kuondosha usumbufu wa utoaji wa matibabu hayo uliopo sasa.

Akitoa ufufanuzi kuhusu kusitisha ujenzi wa jengo hilo Mkurugenzi wa mamlaka ya uhifadhi wa Mjimkongwe Issa Sariboko Makarani amethibitisha kuzuia ujenzi wa jengo hilo kwa vile unaweza kupoteza hadhi ya miji ya kihistoria ya urithi wa kimataifa.

0 comments:

Post a Comment