Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan amezindua rasmi mbio za
Mwenge wa Uhuru kwenye Uwanja wa Jamhuri Mkoani Morogoro leo.
Katika uzinduzi huo amesema utumbuaji
majipu unalenga kuleta matumaini kwa wananchi ambao wamekata tamaa na kuleta
heshima kwa wananchi waliodharauliwa.
Amemnukuu Baba wa
Taifa Mwl Julius Nyerere akisema kuwa nia ya Mwenge wa Uhuru tangu mwanzo ni
kumulika mipaka ya nchi yetu dhidi ya maadui, kuleta matumaini pale ambapo
hakuna matumaini, kuondoa chuki pale ambapo kuna chuki na kuleta heshima pale
ambapo kuna dharau.
Hhivyo dhana ya Mwenge huo inaendana na dhana ya kutumbua
majipu katika Serikali ya awamu ya tano.
“Kaulimbiu ya mbio ya za mwenge mwaka huu ni hii: Vijana ni
nguvu kazi ya taifa, washirikishwe na wawezeshwe,”
Amezitaja baadhi ya
sababu au changamoto zinazowakabili vijana nchini kuwa ni ukosefu wa ajira,
uwezo mdogo wa kuajiri, ukosefu wa mitaji rafiki kwa vijana, maeneo ya kufanyia
kazi pamoja na mitazamo hasi kwa baadhi ya vijana katika kuchagua kazi.
Makamu wa Rais pia amewataadharisha vijana juu ya ongezeko
la kubwa la maambukizi ya ukimwi na matumizi ya madawa ya kulevya na kueleza
kuwa matatizo hayo pia zinaongeza mzigo kwa jamii na serikali katika kuwatibu,
kuwahudumia na kuongezeka kwa vifo.
Kwa upande wake, Waziri Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu Jenista
Mhagama, amemtambulisha George Jackson Kijimba kuwa ndiye kiongozi wa mbio za
mwenge mwaka huu akisaidiana na wakimbiza mwenge wengine watano na
ukimbizaji mwenge huo wa uhuru zitaishia mkoani Simiyu tarehe 14 Oktoba mwaka huu.
0 comments:
Post a Comment