November 23, 2015

Zanzibar inatarajiwa kuwa mwenyeji wa mkutano mkuu wa mwaka wa Jumuiya ya Mawakili wa nchi za Afrika Mashariki.
Mkutano huo utakaofanyika hapa Zanzibar kuanzia Novemba 27 hadi 28 mwaka huu utaratibiwa na chama cha WANASHERIA Mawakili Zanzibar ZLS.
Katibu wa chama hicho Omar   Said   Shaaban amesema kuwa mkutano huo unatarajiwa kuwa na washiriki 400 kutoka nchi za Tanzania, Rwanda, Burundi, Kenya na Uganda,  utafunguliwa na  jaji mkuu wa Zanzibar Omar Othmani Makungu.
Ameeleza kuwa mijadala mbali mbali ya kisheria itajadiliwa ikiwemo uwezekano wa kuifanya taaluma ya sheria kuwa kichocheo cha biashara na uwekezaji katika nchi za nchi hizo.
Amesema mfumo huo wa kutoa huduma za kisheria unatumiwa na jumuiya mbalimbali  za kisheria duniani ili kuwawezesha wanataaluma kuwa na uwezo wa kipato bila kuwa tegemezi kwa watu wengine.
“Kwa kweli mkutano huo ni fursa ya pekee kwa Zanzibar  kwani unaowakutanisha wataalamu waliobobea katika masuala ya kisheria kutoka nchi hizo shiriki” alisema Said.
Kwa mujibu wa maelezo ya katibu huyo amesema  kupitia mkutano huo watajadili pia uwezekano wa mawakili wa nchi hizo kufanya kazi kwa ushirikiano bila ya mipaka wala vikwazo vya kisheria katika nchi za Afrika  Mashariki .

0 comments:

Post a Comment