Waziri Mkuu wa Tanzania Majaliwa Kassim Majaliwa ameitaka
wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za
Mitaa TAMISEMI kujieleza ni sababu ya
kuchelewa hadi sasa kuanza kazi mradi wa mabasi yaendayo kasi DART.
Amesema anashangazwa na mradi huo katika taarifa zinaonyesha kuwa
umekamilika lakini hadi sasa hajaanza kazi na hajui kinachokwamisha hilo.
Waziri mkuu ameagiza watendaji wote wa wizara ya TAMISEMI, akiwemo
Katibu Mkuu wa Wizara hiyo kufika Ofisini kwake kesho asubuhi kueleza kuchelewa
mradi huo wakati miundombinu imeshakamilika.
Ameyasema hayo alipotembelea
Wizara ya TAMISEMI na kuongea na watendaji wa wizara hiyo huku akiwataka
watendaji kufanya kazi kwa mujibu wa hotuba ya Rais Dkt. John
Pombe Magufuli aliyoitoa Bungeni hivi karibuni.
Akizungumza
na waandishi wa habari mara baada ya kikao hicho Katibu Mkuu wa TAMISEMI Katibu
Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Jumanne Sagini amewaagiza watumishi katika wizara
hiyo kufanya kazi kwa bidii kwa kuzingatia maadili pamoja na kujiepusha na
tabia ya uzembe, uvivu na wizi katika maeneo yao ya kazi.
0 comments:
Post a Comment