
Jeshi la Polisi Tanzania limesema jumla ya watuhumiwa 829 wameuawa wananchi
kinyume cha sheria kuanzia Januari hadi Oktoba mwaka huu.
Idadi hiyo imeongezeka ikilinganishwa na watuhumiwa wanaoshukiwa kujihusisha na vitendo vya uhalifu 785 waliouawa kwa
kipindi kama hicho katika mwaka 2014.
Msemaji wa jeshi hilo, Advera Bulimba amesema hali hiyo imechangiwa na baadhi
ya wananchi kuchukua sheria mikononi kwa kuwapiga, kuwadhalilisha , kuwachoma na
kuwaua.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dare es Salaam Bulimba amesmea jeshi
la polisi linakemea tabia hiyo na limetangaza zawadi kwa mwananchi
atakayerekodi tukio la aina hiyo na kuliripoti polisi.
0 comments:
Post a Comment