
Omar Surur Khalfan, Mwanasheria kutoka ofisi ya Mwanasheria Mkuu Zanzibar.
Utowaji hukumu ndogo kwa kesi za jinai ikiwemo makosa ya ubakaji
imechangia makosa hayo kuripotiwa kila wakati Zanzibar.
Mwanasheria kutoka ofisi ya Mwanasheria
Mkuu Zanzibar (DPP), Omar Surur Khalfan, amesema sheria za mwenendo wa makosa
ya jinai ya mwaka 2004 imeanisha adhabu ya kifungo cha miaka 25 hadi 30 ila
imetoa mwanya wa kupunguzwa adhabu hiyo.
Akiwasilisha mada katika mafunzo
maalumu ya jinsia kwa wanahabari wa vyombo mbalimbali amezitolea mfano
mahakama za mikoa ambazo zinalazimika kutoa adhabu isiyozidi miaka saba
ambayo inaokwamisha kutolewa hukumu sahihi kwa kesi kwa hata za
ukatili wa kimwili.
hata hivyo Surur amefahamisha kuwa
mahakama hizo kwa mujibu wa sheria za mahakama zinahitajika kuomba idhini ya
mahakama kuu ili hukumu ya mrefu zaidi ya uliowekwa.
"Makosa haya ya jinai ni mengi
sana hivyo hakimu wa mikoa wanalazimika kufanya utaratibu huo ili kutoa hukumu
ya kifungo cha zaidi ya miaka 20 hadi 30 ila wengi hawafanyi hivyo ili kuwa
fundisho kwa wengine " amesema .
Akizungumzia uchelewaji wa kufunguliwa
mashatka kwa kesi za udhalilishaji kwa kusubiri uchunguzi wa vinasaba DNA
amesema ushihidi huo si lazima kama itakuwepo taarifa ya dakrtari na taarifa
maelezo hasa kwa mtoto chini ya miaka 14 aliefanyiwa vitendo hivyo vya ubakaji.
“Kwahiyo vikwazo hivyo vya kisheria,
usuluhishi nje ya mahakama, adhabu ya faini huku kukiwa na mazingira yote ya
kumtia hatiani mtuhumiwa inazidisha matukio ya ubakaji na hata kuongeza ndoa za
umri mdogo zanzibar”… aliwaarifu wanahabari hao .
Ameshauri kufanyika marekebisho ya
haraka kwa baadhi ya sheria zilizopitwa na wakati ili kuziba mianya kwa baadhi
ya watendaji wa vyombo vya sheria na kutoa hukumu haraka katika kutoa haki kwa
waathirika wa matukio hayo kwa wakatii uliopo.
Amezitaja sheria hizo ni ushahidi, ya
ndoa, sheria ya vizazi na vifo na sheria ya watoto iliyofanyiwa marekebisho
mwaka 2011.
Nao washiriki wa mafunzo hiyo
walipendekeza kwa Serikali kupitia vyombo vyake vya sheria kuzuia dhamana kwa
watuhumiwa wa matendo ya ubakaji yanaoripotiwa katika vuombo vya sheria.
"Kunyimwa dhamana pekee ni adhabu
lakini kama mtuhumiwa anapewa anaweza kufanya tena kwa kuhisi kuwa hakuna
adhabu itakakayomkabili", amesema Issa Yusuf wa Daily news.

Baadhi ya washiriki wakiskiliza kwa makini
Husna Mohamed wa gazeti la Zanzibar leo
kwa upande wake amedai kuwa sheria ya elimu na ndoa lazima zifanyiwe
marekebisho hayo kwani inatoa mwanya wa kutoa haki kwa wanafunzi waliopewa ujauzito
au kuolewa kupata haki zao.
“Kwahiyo vikwazo hivyo vya kisheria,
usuluhishi nje ya mahakama, adhabu ya faini huku kukiwa na mazingira yote ya
kumtia hatiani mtuhumiwa inazidisha matukio ya ubakaji na hata kuongeza ndoa za
umri mdogo zanzibar”… aliwaarifu wanahabari hao .
Ameshauri kufanyika marekebisho ya
haraka kwa baadhi ya sheria zilizopitwa na wakati ili kuziba mianya kwa baadhi
ya watendaji wa vyombo vya sheria na kutoa hukumu haraka katika kutoa haki kwa
waathirika wa matukio hayo kwa wakatii uliopo.
Amezitaja sheria hizo ni ushahidi, ya
ndoa, sheria ya vizazi na vifo na sheria ya watoto iliyofanyiwa marekebisho
mwaka 2011.
Nao washiriki wa mafunzo hiyo
walipendekeza kwa Serikali kupitia vyombo vyake vya sheria kuzuia dhamana kwa
watuhumiwa wa matendo ya ubakaji yanaoripotiwa katika vuombo vya sheria.
"Kunyimwa dhamana pekee ni adhabu
lakini kama mtuhumiwa anapewa anaweza kufanya tena kwa kuhisi kuwa hakuna
adhabu itakakayomkabili", amesema Issa Yusuf wa Daily news.
Baadhi ya washiriki wakiskiliza kwa makini |
Husna Mohamed wa gazeti la Zanzibar leo
kwa upande wake amedai kuwa sheria ya elimu na ndoa lazima zifanyiwe
marekebisho hayo kwani inatoa mwanya wa kutoa haki kwa wanafunzi waliopewa ujauzito
au kuolewa kupata haki zao.
0 comments:
Post a Comment