April 12, 2014

zenjkijiwe.blogsopt.com
Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Uhifadhi wa Mji Mkongwe Mohammed Baloo na Msimamizi Mkuu wa Jumuiya ya ACRA nchini Tanzania Nicola Morganti wakitia saini ya Makubaliano ya Mradi wa Uhifadhi wa Urithi wa Zanzibar na Kutengeneza Ajira (Zanzibar Built Heritage for Job Creation) mjini Zanzibar
 Jumla ya watu elfu kumi na tano mia tisa najuhimko ishirini na mbili watafaidika na Mradi wa uhifadhi wa urithi wa Zanzibar na kutengeneza  ajira utakaogharimu euro milioni 1,200,000 sawa na zaidi ya shilingi bilioni moja za tanzania.
Mradi huo wa miaka mitatu unatekelezwa na Jumuiya ya Uhifadhi wa Mji Mkongwe (JUHIMKO) kwa kushirkikiana na jumuiya ya ACCRA (Cooperanzione in Afrika e America Latin).
Akizungumza katika hafla ya utiaji saini mjini Zanzibar Mwenyekiti wa JUHIMKO Muhammed Bhaloo amesema mradi huo unalenga kuutunza na kuutangaza urithi wa kiutamaduni uliopo Zanzibar ili kuchangia ukuaji wa uchumi.
“Walengwa wakuu wa mradi huo ni pamoja na mafundi ujenzi, wajasiriamali, wamiliki wa majengo ya umma na binafsi, watembeza watalii, walimu 200 na wanafunzi 10,000 wa skuli za msingi na sekondari  pamoja na wananchi wa kawaida”.amefahamisha Bhaloo.
Ameeleza kuwa kutatolewa na mafunzo ya muda mfupi ya ujenzi na usimamizi wa uhifadhi wa mjengo ya kihistoria, kuanzishwa maabara katika chuo kikiu cha taifa suza na  kuandaliwa mtaala ya kufundisha matengenezo ya majengo ya kale na mengine utakaotumia katika chuo cha karume.
Amesema JUHIMKO  itakuwa msimamizi mkuu wa shuhuli za kutoa taaluma na uelewa kwa walengwa juu ya historia na urithi wa kitamaduni wa mji mkongwe wa Zanzibar ni miongoni mwa miji ya urithi wa kitaifa inayotambuliwa na UNESCO.
Msimamzi wa mkuu wa jumuiya ACRA Nicola Morganti ameshukuru uongozi wa JUMHIKO kwa hatakati zao za kuhifadhi historia na utamaduni wa Zanzibar.

0 comments:

Post a Comment