April 30, 2014

Taasisi inayosimamia mambo ya kale na harakati za Siti binti Sadi inakusudia kujenga kituo cha kumbu kumbu katika kijiji cha fumba ikiwa ni hatua ya kuwaenzi wasanii wa Zanzibar.
 Katibu wa taasisi hiyo Khamis Mohamed Juma amesema hatua hiyo ni kumuezi  msaani huyo alizaliwa  katika kijiji hicho mwaka 1880. na kuendeleza historia za wasanii wengine ili kutoa elimu kwa  jamii.
 Amehamaisha kuwa taasi hiyo imeamua kukusanya na kuzihifadhi kumbu kumbu za Siti binti Sadi kutokana na mchango mkubwa alioutoa  ikiwemo kutetea haki za binaadamu Zanzibar.
Ameeleza hayo katika ziara ya kamati hiyo iliyotembelea katika  kijiji hicho cha Fumba  wilaya Magharibi Unguja.
Mmoja wa ndugu wa familia wa marehemu Muharam Mohamed akielelzea  historia ya siti bint sadi amesema alikuwa ni mfano mzuri wa kuigwa na wasanii wengine wa kizazi kipya  kwani alitumia fani ya uimbaji katika kukuza maadili ya Zanzibar.
Siti binti Sadi alikuwa ni msanii wa kwanza mkubwa wa kurikodi Taarab aliifanya Taarab kuwa maarufu kutokana na nyimbo zake za mapenzi zilizobeba ujumbe kwa kijamii na uchambuzi wa kisiasa na zimesaidia kukuza lugha ya kiswahili katikanchi mbali mbali za Afrika ya Mashariki

0 comments:

Post a Comment