February 05, 2016


Zanzibar bado inakabiliwa na tatizo la saratani huku kukisekana mipango bora ya kukabiliana na ugonjwa huo.
Mwenyekiti wa jumuiya ya watu wanaoishi na saratani Zanzibar MSAFIRI MARIJANI amezitaja changamoto hizo ni pamoja na ukosefu wa wataalamu wa Magonjwa hayo  katika vituo vya afya, ukosefu wa vifaa na dawa za tiba na uelewa ni mdogo wa jamii juu ya kujikinga na saratani.
Akizungumza na waandishi wa habari ikiwa ni maadhimisho ya siku ya ugonjwa huo duniani amesema Zanzibar haina takwimu kamili ya wagonjwa wa kisukari lakini kiasi ya watu 1000 kutoka visiwani huo wanapokelewa kila mwaka katika hospitali ya ocean road kwa  matibabu.
Amefhamisha kuwa saratani ya matiti na shingo ya kizazi  ndizo  zinaongoza kwa   wanawake Zanzibar na saratani ya tenzi dume inaongoza kwa  upande wa wanaume.
Dkt Marijani ambae pia ni daktari dhamana wa Magonjwa hayo Zanzibar amefahamisha kuwa  tiba za ugonjwa huo ni ghali sana ila njia pekee ni jamii kubadilisha  mfumo wa maisha ikiwemo kupunguza kula vyakula vya mafuta,  kufanya mazoezi, kuache pombe na uvutaji wa sigara unaochangia asilimia 40 ya aina za saratani.
“Saratani  inaweza kuzuilika  iwapo itawahiwa mapema, tuongezeni nguvu kukabiliana nayo  vyenginevyo inaweza kuathiri wananchi wengi kwani gharama ya matibabu yake ni kubwa na wagonjwa  wengi  hushindwa na kupoteza maisha,” amesisitiza Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo.
Amewakumbusha wananchi kuwa saratani ni uvimbe mpya kwenye mwili na baada ya muda mfupi  huzalisha chembechembe  zinazosababisha athari kubwa na kama haikuwahiwa mapema inasababisha donda kubwa na kuwa halitibiki tena.
Nae mkurugenzi wa utumishi Wizara ya Afya Zanzibar Omar Mwinyi Kondo amesema mapambano ya ugonjwa saratani unahitaji mikakati endelevu huku akiomba jumuiya hiyo kutochoka kuelimisha  jamii juu ya  ugonjwa huo
Akitoa ufafanuzi kuhusu mkakati wa kukabiliana na matumuzi ya tumbaku Zanzibar ambayo ni miongoni mwa chanzo kikuu cha ugonjwa huo Mratibu wa kitengo cha maradhi yasiyoambukiza Wizara ya Afya Zanzibar  Zuhura Saleh Ame amesema mkakati wa kuanzisha sheria ya matumuzi na usimamizi wa tumbaku unaendelea kutokana na matumuzi yake kuongezwka kwa kadi Zanzibar
Kauli mbiu ya siku ya Saratani inayoashimishwa kila ifikapo April 4 ya kila mwaka ni MIMI NA WEWE TUNAWEZA KUJIKINGA NA SARATANI.

Mkurugenzi wa Utumishi na uendeshaji Wizaraya ya Afya Zanzibar Omar Mwinyi Kondo
 akizungumza na waandishi katika maadhimisho ya siku ya saratani duniani
 yaliyofanyika Ofisi ya Jumuiya Mpendae.

Viongozi ya Maradhi ya Saratani wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi
katika maadhimisho ya siku ya saratani duniani ndugu Omar Mwinyi Kondo (kati)
mwenye suti na baadhi ya viongozi na waandishi wa habari waliohudhuria.

0 comments:

Post a Comment