December 17, 2015

Aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Tanzania Jaji mstaafu Mark Boman amemuomba aliyekuwa mgombe uraisi kwa tiketi ya chama cha wananchi CUF Maalimu Seif Sharifu  Hamadi kukubali uamuzi wa kurudiwa kwa uchaguzi mkuu Zanzibar.
Amesema ni vyema akubali maamuzi hayo kwani kama alishinda atashinda tena kwa vile waliompigia kura katika uchaguzi ulifoutwa ni wale wale watakao mpigia tena na wanaweza kuongezeka.
Boman ameyasema hayo jijini dar es salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari amesema kuwa maalim kujitangazia kuwa ameshinda ni suala lilokuwa halikufuata utaratibu hivyo nivyema uchaguzi ufanyike ili kupata rais wa serikali ya zanzibar.
Aidha amesema ili kumaliza mgogoro huo kurudiwa uchaguzi ni suluisho pekee lakini ni muhimu kuwepo masharti ya haki, uwazi pamoja na wagombe na vyama vyao waahidi kukubali matokeo ya uchaguzi utakaorudiwa .                                    
Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi Zanzibar Jecha Salum Jecha ilifuta matokeo ya uchaguzi huo uliofanyika visiwani humo  kutokana  na madai ya kasoro mbalimbali zilizojitokeza.

Akizungumzia kuhusu mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya ya Tanzania Jaji mstaau Bomani amesema mchakato  huo unatakiwa kuendelea mara moja ili kukamilisha kazi hiyo.

0 comments:

Post a Comment