April 18, 2016

Mtu mmoja amefariki na zaidi ya nyumba mia tisa zimethirika kufuatia mvua kubwa iliyonyesha kisiwa cha unguja usiku wa kumkia jana.
Waziri wa nchi afisi ya Makamu wa Rais Aboud Mohamed Aboud amesema mtu huyo Salim Mohamed Kindi mkaazi wa Migombani ngazi mia amefariki kwa kuangikiwa na ukuta wa nyumba yake.
Akitoa taarifa kuhusu athari za mvua hizo katika mkoa wa mjini magharibi amesema kutokana na kasi ya maji ya mvua nyumba nyengine zimebomoka, zimenguka hali iliyowafanya baadhi ya watu kuyahama makaazi yao huku na miundo mbinu kadhaa ya barabara imeharibika.
Waziri aboud amesema serikali inaendelea kuchukuwa juhudi za kuwasiaida walioathirika na mvua hizo na inatarajia kufungua kambi za wahanga mafuriko ya mvua hizo katika maeneo mbali mbali ya mji.

Akizungumzia hatau za za baadae za kubaliana  na  mafuriko yanayotokea kila ifikapo msimu wa mvua amesema serikali inakusudia kubomoa nyumba zote zilizojengwa katika njia za maji na mabondeni na katika hatau za awali kiasi nyumba mia tatu zitabomolewa na wakazi watapewa maaeneo ili kujenga nyumba.




0 comments:

Post a Comment