Kamati Kuu ya Taifa ya sensa ya watu
na makazi ya mwaka 2012 Tanzania inatarajia kuzindua chapisho la tatu la
taarifa za msingi za kieneno, kijamii na kiuchumi .
Amezipongeza taasisi na mashirika ya kitaifa na kimataifa kwa kusaidia kufanikisha kazi ya sensa hasa katika upatikanaji wa fedha.
Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa
kuzindua chapisho hilo tarehe 23 mwezi huu katika ukumbi wa Kimataifa wa Julius
Nyerere jijini Dar es salaam ikiwa ni maadhimisho ya miaka 50 ya muungano wa Tanzania
.
Mwenyekiti mwenza wa kamati HIYO Balozi
Seif Ali Iddi ametoa taarifa hiyo katika kikao cha kamati hiyo ya sensa huko
Dodoma.
Akitoa taarifa ya Wizara ya fedha ya Serikali
ya tanzania Naibu Waziri mh. Muigulu Nchemba amesema wizara hiyo inaendelea na maandalizi ya
machapisho mengine 10 kuhusu vizazi na ndoa, elimu, uhamiaji na makazi pamoja
na hali ya ulemavu kupitia ripoti hiyo ya sensa.Amezipongeza taasisi na mashirika ya kitaifa na kimataifa kwa kusaidia kufanikisha kazi ya sensa hasa katika upatikanaji wa fedha.
“ …tunawashukuru wadau wetu wa
maendeleo kwa kweli wametusaidia
kutuunga mkono katika zoezi hilo kwa zaidi ya shilindi bilioni tatu “. amesema Mh.
Nchemba.
Nae Mkurugenzi Mkuu wa ofisi ya
taifa ya takwimu Tanzania Dr. Albina Chua akitoa taarifa amesema wamefanya kazi
ya uhakiki wa mipaka ya wilaya za Tanzania bara na Zanzibar katika
wilaya za Gairo na Chemba kwa Tanzania bara na Wete na Micheweni kwa
upande wa Zanzibar.
![]() |
Baadhi ya Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambao ni Wajumbe wa KamatiI Kuu ya Taifa ya Sensa Tanzania wakiendelea na Kikao chao Mjini Dodoma. |
0 comments:
Post a Comment